Fani ya Fasihi Simulizi, kwa Gredi ya 10, 11 na 12 kimeandikwa kwa utaalamu mkubwa ili kufanikisha kikamilifu ufundishaji na ujifunzaji wa fasihi simulizi katika kiwango hiki. Kitabu hiki kimeshughulikia kwa kina na kwa njia ya wazi na nyepesi tanzu na vipera vya fasihi simulizi katika mtaala wa Gredi ya Kumi hadi Gredi ya Kumi na mbili.
Katika kitabu hiki, utapata:
- Ufafanuzi wa kina wa dhana ya fasihi kwa jumla na hususan fasihi simulizi.
- Uchanganuzi wa kina wa tanzu na vipera lengwa vya fasihi simulizi na mifano maridhawa.
- Tungo za kuchangamsha, kusisimua na vilevile kurahisisha ujifunzaji.
- Shughuli zenye kushirikisha kikamilifu katika ujifunzaji.
- Tathmini endelevu za kumwezesha mwanafunzi kujitathmini na kutathminiwa na wenzake au na mwalimu.
- Tathmini ya mwisho wa sura ili kumpa mwanafunzi picha ya jumla kuhusu kiwango chake cha ufahamu wa utanzu na kipera husika.
- Mazoezi murua yanayochochea ujifunzaji huku yakipima ngazi zote za maarifa au utambuzi.
- Majaribio ya Tathmini yenye mazoezi na maswali anuwai yatakayomwezesha mwanafunzi kupima umilisi wake.
- Majibu kwa Majaribio ya Tathmini ili kumwelekeza mwanafunzi kubuni mikakati ya kujiboresha.







Reviews
There are no reviews yet.